KUTOKA MAHAKAMANI HAI – KILIMANJARO

KUTOKA MAHAKAMANI HAI – KILIMANJARO

Mei 29, 2023 Shauri la Uhujumu Uchumi Na 4.2023 dhidi ya Afisa wa TANESCO Bw. DAVID KISEY lilifunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya Hai. Mshtakiwa anakabiliwa na makosa 3 ambayo ni ubadhirifu, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu na matumizi mabaya ya mamlaka . Mshtakiwa akiwa mwajiriwa wa TANESCO kwa vipindi tofauti tofauti mwaka 2022, alijipatia kiasi cha sh. 760,000= kutoka kwa mteja akimdanganya kwamba angempatia huduma ya umeme. Aidha mshtakiwa amekana makosa yote na yupo nje kwa dhamana. Shauri…

Read More Read More

KUTOKA MAHAKAMA YA WILAYA YA MWANGA – KILIMANJARO

KUTOKA MAHAKAMA YA WILAYA YA MWANGA – KILIMANJARO

Mei 29, 2023, katika Mahakama ya Wilaya ya Mwanga limefunguliwa Shauri la Uhujumu Uchumi namba 2/2023, ambapo washtakiwa ni 1. Zefrin K.Lubuva (aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji H/W Mwanga), 2.Mwajuma H.Muna (aliyekuwa Mhasibu Msaidizi wa Mji Mdogo Mwanga) 3.Hassan A.Hassan (aliyekuwa Kaimu Mweka Hazina wa H/W Mwanga) na 4.Regnald P. Massawe (Kaimu Afisa Mtendaji Mamlaka ya Mji Mdogo Mwanga) kwa makosa ya matumizi ya nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri (washtakiwa wote) na matumizi mabaya ya mamlaka (mshtakiwa wa kwanza). Washtakiwa hao…

Read More Read More

KUTOKA MAHAKAMA YA WILAYA SONGWE

KUTOKA MAHAKAMA YA WILAYA SONGWE

Juni 01, 2023 imefunguliwa Kesi ya Uhujumu Uchumi namba ECO. 04/2023 katika Mahakama ya Wilaya ya Songwe, mbele ya Mh. Lugome. Kesi hiyo ni Jamhuri dhidi ya Lington Mbuzi, Mkusanya Mapato katika H/W ya Songwe, Mkoani Songwe. Hati ya Mashtaka imesomwa na Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU Conrad Kabutta kwamba kati ya tarehe 06.05.2017 na 10.10.2019, Mshtakiwa akiwa na nia ovu alitumia madaraka yake vibaya kwa kushindwa kupeleka fedha kwa Mhasibu wa H/W ya Songwe au kuweka kwenye akaunti ya H/W…

Read More Read More