WIKI YA SHERIA 2025 – DODOMA

WIKI YA SHERIA 2025 – DODOMA

” Ninawapongeza sana TAKUKURU katika kutekeleza jukumu la kuzuia rushwa. Ninashauri muweke nguvu zaidi katika kuelimisha viongozi wa dini, kwani wananchi wakihubiriwa pia rushwa ni dhambi na ikawaingia mioyoni mwao watakuwa na mwenendo mwema na watabadili tabia hivyo vitendo vya rushwa vitapungua”. Haya yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Prof. Elisante Ole Gabriel, alipotembelea banda la TAKUKURU katika viwanja vya Nyerere Square – Jijiji Dodoma, Januari 27, 2025.

WIKI YA SHERIA – 2025 IRINGA

WIKI YA SHERIA – 2025 IRINGA

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh. Peter Serukamba (kati), ametembelea banda la TAKUKURU katika Maonesho ya Wiki ya Sheria na kuipongeza TAASISI kwa kushirikiana na WADAU katika Kuzuia Rushwa. TAKUKURU Iringa.Januari 25, 2024

WIKI YA SHERIA 2025 – UVINZA

WIKI YA SHERIA 2025 – UVINZA

“Vitendo vya Rushwa ya Ngono vinaathiri ukuaji na ufanisi wa utoaji wa huduma hasa kwa vijana ambao ndio nguzo ya Taifa. Msikubali kunyanyasika! Hakikisheni mnakuwa jasiri wa kutoa taarifa kupitia namba 113 mapema pindi unapoona vitendo hivi vya Rushwa katika jamii au shuleni.” Hayo yamesemwa na Bi. Mwasity Mshana alipokuwa akielimisha wanafunzi Kata ya Nguruka katika maadhimisho ya siku ya Sheria. TAKUKURU UVINZA Januari 25, 2025