WAKALA WA VIPIMO SONGWE WAELIMISHWA KUHUSU MAADILI MAHALA PA KAZI.
“Kazi zenu ni nyeti kwa ustawi na usalama wa nchi, hivyo ni muhimu kwenu kuzingatia maadili wakati wote mnapofanya kazi zenu”. Hayo yamesemwa na Naibu Mkuu wa TAKUKURU (M) wa Songwe Bw Mohamed Shariff (aliyekaa kushoto mbele), wakati akitoa semina ya umhimu wa kuzingatia maadili mahala pa kazi kwa watumishi wa Wakaka wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Songwe. Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Songwe Bw. Siraji Moyo ameishukuru TAKUKURU kwa elimu na kuahidi kutoa ushirikiano…