WAKALA WA VIPIMO SONGWE WAELIMISHWA KUHUSU MAADILI MAHALA PA KAZI.

WAKALA WA VIPIMO SONGWE WAELIMISHWA KUHUSU MAADILI MAHALA PA KAZI.

“Kazi zenu ni nyeti kwa ustawi na usalama wa nchi, hivyo ni muhimu kwenu kuzingatia maadili wakati wote mnapofanya kazi zenu”. Hayo yamesemwa na Naibu Mkuu wa TAKUKURU (M) wa Songwe Bw Mohamed Shariff (aliyekaa kushoto mbele), wakati akitoa semina ya umhimu wa kuzingatia maadili mahala pa kazi kwa watumishi wa Wakaka wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Songwe. Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Songwe Bw. Siraji Moyo ameishukuru TAKUKURU kwa elimu na kuahidi kutoa ushirikiano…

Read More Read More

UFUATILIAJI WA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO – LINDI

UFUATILIAJI WA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO – LINDI

“Tunaishukuru Serikali kwa kumaliza kero yetu ya kukosa Shule ya Sekondari kwenye kata yetu iliyopelekea watoto wetu kusafiri umbali wa km 20 kwenda shuleni huku usafiri ukiwa wa shida sana. Pia tunaipongeza TAKUKURU kwa ufuatiliaji wa utekelezaji wa mradi huu na kutukumbusha majukumu na wajibu wetu katika kuzuia vitendo vya rushwa pamoja na umuhimu wa kutoa taarifa ili zifanyiwe kazi kwa wakati. Tunazidi kutumia elimu ya rushwa tunayoipata kuelimisha na wengine.” Hayo yamesemwa na Bw. Yakobo Chaime Maundi, Mjumbe wa…

Read More Read More

WANAFUNZI SHULE YA MSINGI BUIKO WAPATIWA ELIMU YA RUSHWA NA MAADILI WILAYANI KOROGWE.

WANAFUNZI SHULE YA MSINGI BUIKO WAPATIWA ELIMU YA RUSHWA NA MAADILI WILAYANI KOROGWE.

“Mwanafunzi mwenye maadili ni yule ambaye ana adabu na ni mtiifu kwa wazazi na waalimu, mwenye bidii katika kazi zote shuleni na nyumbani na pia hajihusishi na vitendo vyenye kuashiria tabia mbaya au utovu wa nidhamu”. Ni nukuu katika maelezo ya Rukia Omari (aliyesimama), mwanafunzi wa Shule ya Msingi Buiko alipoeleza mwenendo wa mwanafunzi mwadilifu alipotakiwa kufanya hivyo baada ya kuelimishwa. Mada iliwasilishwa na Mkuu wa TAKUKURU (W) ya Korogwe Bw. Raymond Katima, Novemba 28, 2023.