WIKI YA SHERIA 2025 – DODOMA
” Ninawapongeza sana TAKUKURU katika kutekeleza jukumu la kuzuia rushwa. Ninashauri muweke nguvu zaidi katika kuelimisha viongozi wa dini, kwani wananchi wakihubiriwa pia rushwa ni dhambi na ikawaingia mioyoni mwao watakuwa na mwenendo mwema na watabadili tabia hivyo vitendo vya rushwa vitapungua”. Haya yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Prof. Elisante Ole Gabriel, alipotembelea banda la TAKUKURU katika viwanja vya Nyerere Square – Jijiji Dodoma, Januari 27, 2025.